Sunday, October 9, 2016

WANAOKUMBATIA MASHAMBA MORO KUPOKONYWA.

SERIKALI mkoani Morogoro imetoa wiki mbili kwa uongozi wa halmashauri ya Malinyi,kuchukua uamuzi wa kuwapokonya mashamba wananchi ambao wamekumbatia mashamba katika skimu ya Umwagiliaji ya  Alabama bila kuyaendeleza.

Mashamba hayo yatolewa upya kwa wananci wenye uhitaji wa kuendeleza kilimo katika Skimu hiyo,kwani hakuna haja ya kukumbatia ardhi wakati kuna wengine wanahitaji kuendeleza kilimo.

Mkuu wa Morogoro Dr Kebwe Stephen, alisema haiwezekani serikali imepoteza zaidi ya bilioni 6 kwa ajili ya kuwajengea Skimu hiyo, lakini jambo la ajabu kuna baadhi ya wananchi wamekaa na mashamba bila kuyaendeleza, wakati wapo vijana ambao wanataka kujihusisha na kilimo katika mashamba hayo hata kwa kukodishiwa.

Alisema serikali ilitoa kiasi cha shilingi billion 6 kwa ajili ya ujenzi wa skimu hii ya umwagiliaji, mradi ambao unafursa pekee kwa wakazi wa Itete na wilaya Malinyi, kufanya kilimo cha mazao mbalimbali msimu mzima wa mwaka.

Mkazi wa Itete,Salum Mkola aliiomba serikali kuwawezesha katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili, hususani katika upande wa  elimu, juu ya kilimo cha umwagiliaji,kwani kuna baadhi wameshaanza kufaidika na kilimo hicho,huku wengine wakikosa ujuzi wa kilimo cha kisasa.

Makamu Mwenyekiti Halmshauri ya Malingi,Severus Kamguna alisema kero za wakulma zinashughulikiwa pamoja na  kuwaondoa wale wote wanaoendelea kukumbatia mashamba hayo bila kuyaendeleza.

Skimu ya umwagiliaji ya Alabama ina jumla ya hekta 8000 lakini mpaka sasa ni ekari 1800  ambazo  zinazotumika kwa kilimo na shughuli za kilimo hufanyika kipindi chote cha mwaka.


Mwisho..

No comments:

Post a Comment