Sunday, October 9, 2016

WAGONJWA WAPATA HUDUMA YA AFYA CHINI YA MTI,KISA KUKOSA ZAHANATI

          

MAMA wajawazito na wenye watoto wadogo katika kata ya Mindu Manispaa ya Morogoro wamelzimika kupata huduma ya afya,chini ya mti kutokana na kukosekana huduma ya kituo cha afya na zahanati kwa kipindi cha muda mrefu.

 Kundi kubwa la kinamama wenye watoto wachanga kutoka  ya mitaa nane ya kata ya Mindu wameonekana na wakipata huduma za kliniki na chanjo chini ya mti katika ofisi ya kata hiyo.

 Aidha akina mama hao walionekana wakiwa wamekaa chini ya miti kukiwa hakuna benchi wala viti vya kusubiria huduma wakati wakiitwa mmoja mmoja kupata huduma hiyo.

Mama Sharifa Duttilo alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakiomba kujengewa Zahanati lakini hakuna juhudi zozote kutoka kwa viongozi wao zinazoonekana kufanyika wala kuhamasisha wananchi kufanya ujenzi huo.

Sharifa anaiomba halmashauri,serikali kuu,na wadau wengine wa maendeleo kuwasaidia ujenzi wa zahanati,kituo cha afya ili kupunguza adha wanayoipata ya huduma ya afya kwa muda mrefu,ambayo wakati mwingine kukosa tiba za afya kunaweza sababisha madhara makubwa zaidi.

Afisa mtendaji kata ya Mindu Laurent Masanja alisema tayari wameunda kamati ya uhamasishaji kusaidia kukusanya michango mbalimbali kutoka kwa wananchi na wadau wengine ili kukabiliana na changamoto hiyo ya zahanati.

Masanja alisema kamati hiyo imeundwa ili kuwataka wananchi wenyewe kujitokeza, kuanza ujenzi kabla ya wadau wenguine kujitokeza,wakati wakisubiri fedha kutoka halmashauri.

Diwani wa kata Mindu Hamis Msasa akisema changamoto hiyo imekuwa ni ya muda mrefu lakini wamejitahidi kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto ingawa kikwazo bado ni upatikanaji wa fedha za ujenzi.

Msasa alisema kwa kushirkiana na viongozi wa mitaa 8 husika wanajipanga kumaliza kilio hicho cha afya, kwani hakuna kiongozi anapenda wananchi wake wateseke,hivyo aliwataka wananchi kujitokeza kuchangia ujenzi wa kituo cha afya pindi utakapoanza.

Kata ya mindu iliyopo Manispaa ya Mororogoro ina jumla ya wakazi 2384,shule za msingi 4,zahanati 1,hospitali 1 ya Mazimbu

No comments:

Post a Comment