Monday, September 26, 2016

WATOTO 6OO WAKOSA FURSA YA ELIMU KILOMBERO


LICHA ya serikali ya awamu ya tano kutoa fursa ya elimu,hali imekuwa tofauti kwa watoto zaidi ya 600 Kitongoji cha Namwawala B wilayani Kilombero, ambapo wamekosa fursa tokana na umbali uliopo toka katika kitongoji hicho hadi shule ilipo.

Wakizungumza katika mkutano ulioitishwa na Mkuu Wa wilaya ya Kilombero James Ihunyo,wakazi wa eneo la Mikochini katika kitongoji cha Namwawala wamesema wapo katika eneo hilo kwa miaka 15 sasa bila Huduma muhimu za kijamii ikiwemo shule.

Walisema kwa sasa eneo la Mikochini lina watoto 600 wanaojisomea katika kibanda kidogo kwa walimu wa kujitolea huku wengine wakitembea umbali Wa kilomita 18 kufuata elimu katika kitongoji cha Idandu.

Madalu Basu mkazi Wa Mikochini alisema wamefuatilia suala hilo kwa muda mrefu bila mafanikio na kufanya watoto wengi kukosa fursa ya elimu hali inayopelekea kuwafanya watoto hao kuwa kuolewa mapema ama kuwa wachungaji.

 Sambamba na shule pia wananchi hao walisema eneo hilo halina uduma nyingine za msingi kama maji,zahanati na barabara na kuwafanya wananchi hao wajione kama wapo katika giza.

Akizungumzia suala la kukosa zahanati,Daniana Rajabu alisema kuwa hali hiyo inapelekea akinamama wengi wajawazito kujifungulia njiani na inawapa wakati mgumu kwenda kijijini Namwawala kwani inawabidi kuvuka mito miwili ili kufikia zahanati.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Namwawala B,Machia Nyambu alisema kwa sasa wakazi Wa Mikochini wapo 4000 na wanaiomba serikali kuwasajili ili kupata kijiji kutokana na kuwa na sifa zote na baada ya kupata kijiji Huduma zote muhimu zitapatikana hasa kutokana na wananchi wa eneo hilo kuwa na moyo wa kujitolea.

Nyambu alisema kwa kuanzia wananchi hao wamejenga boma kwa ajili ya kliniki NA pia kujenga darasa la miti huku pia wakichimba Barbara ya kilomita tano kwa kujitolea NA kusema kuwa serikali ikiwaunga mkono katika kuwajengea shule wao wapo tayari kuchangia shilingi laki tano kwa kila mmoja ili kukamilisha.

Mkuu Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo alisema kuna haja eneo hilo kuwepo shule ya msingi hasa baada ya kubaini uwepo wa watoto wengi na atatuma wataalamu wa elimu kufika eneo hilo na kufanya tathmini ili mwaka 2017 watoto waanze shule.


Kuhusu ombi la kupatiwa kijiji,Ihunyo alisema kuwa taratibu zinabidi zifuatwe kuanzia ngazi za chini ila amesisitiza kuwa kinachotakiwa kwa sasa ni kupatiwa Huduma muhimu ikiwemo maji,zahanati na shule.

No comments:

Post a Comment