JESHI la
Polisi Mkoani Morogoro linamshikilia mwanamke Anna Luambano (33) mkazi wa Kipawa jijini Daressalam kwa kosa la kuiba mtoto
mwenye umri wa siku 10 aliyefahamika kwa jina la Angel Meck mkazi
wa Chamwino Manispaa ya Morogoro.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Ulrich Matei alisema kuwa
tukio hilo lilitokea Septemba 13
majira ya asubuhi ambapo
askari polisi walipata taarifa za kuibiwa kwa mtoto huyo kutoka kwa mama wa
mtoto huyo aliyefahamika kwa jina la Maimuna Mahmudu (20) huko maeneo ya Kilimahewa.
Kamanda Mtei alisema kuwa mtuhumiwa
huo alikamatwa akiwa njiani maeneo ya Mdaula akiwa anelekea Dar es salaam anakoishi mara baada ya kufanikiwa kumdanganya mama
mzazi wa mtoto huyo kutoka
Hospitali ya Kata ya Mafisa kuwa
ampe ili akamuonyeshe
mume wake kuwa mtoto wa mdogo wake amejifungua ili awape fedha za hongera kisha wagawane.
Kamanda huyo alisema kuwa
mtuhumiwa anahojiwa na hatua za kumfikisha mahakamani zinafuata na kuwashukuru wale wote waliotoa ushirikiano hadi
kufanikisha kumkamata
mwizi wa mtoto huyo na
kuwaomba kuendeleza ushirikiano na jeshi hilo ili kukomesha vitendo hivyo.
Kwa upande wake mtuhumiwa wa wizi wa Mtoto huyo aliwaambia
wandishi wa habari kuwa alifanya kitendo hicho baada ya kutafuta kupata mtoto
kwa muda mrefu bila mafanikio licha ya kuomba apewe mtoto kutoka ustawi wa jamii ndipo akaamua kufanya kitendo
hicho ili nae aweze kuwa na mtoto na kuitwa mama.
No comments:
Post a Comment