Sunday, October 16, 2016

NINI KIFANYIKE KUPUNGUZA MIGOGORO YA ARDHI.

                                      
Afisa Programu wa Shirika la Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali linalofanya kazi na wakulima ,wafugaji wadogo Tanzania(PELUM),Angolil Ryson akiongea na wafaugaji wa kijiji cha Mela,kata ya Melela Mvomero.

WANANCHI wa Kijiji cha Mela kata ya Melela Wilayani Mvomero wamesema ili kupunguza migogoro ya ardhi,kila kijiji kipimwe na kuanishwa mipaka,kila mwananchi apimiwe eneo lake analoishi kwa lengo la kuepuka mwingiliano.

Hayo yalibainishwa katika mdahalo uliofanyika katika kijiji cha Mela,uliokuwa unajadili nini kifanyike ili kupunguza migogoro ya ardhi,uliondaliwa na Shirika la Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali yanayofanya kazi na wakulima na wafugaji wadogoTanzania  (PELUM)

Kishakwi Mlimba alisema kuwa migogoro mingi inasababishwa na wananchi kutokujua mipaka ya eneo analomiliki,hivyo kama watapimiwa maeneo yao wanayomikili na kupewa hati miliki kwa kila mmoja itapunguza mwingiliano na kila mtu kujua mipaka yake.
“naomba serikali na wadau kutusadidia kupima kijiji chetu,kiwe kwenye matumizi bora ardhi,hatupendi migogoro ya ardhi itokee kwani inaurudisha nyuma katika shughuli za maendeleo.”Alisema.

Naye Sayota Singa alisema kinachofanya jamii ya wafugaji kuhama hama ni ukosefu wa maji kwa mifugo,na matumizi ya binadamu,hivyo ili kuzuia wafugaji kukaa sehemu moja lazima serikali iweke miundo mbinu mizuri ikiwa ni pamoja na maji ya kudumu kuwepo.

Singa alisema kuwa katika kijiji cha Mela kuna mashamba pori,yapo kwa muda mrefu bila shughuli yoyote,hivyo aliiomba serikali kabla ya kufanya mpango wa matumizi bora ya ardhi mashamba hayo yatambuliwe,ardhi ipo ila idaid ya wananchi inaongezeka kila siku, hivyo ardhi kama haitumiki ipewe wananchi waiendeleze kulikoa kuwa pori

                                
Wananchi wakifuatilia mdahalo.

Kwa upande wake,Afisa Miradi,kutoka PELUM,Rehema Fidelis alisema kuwa lengo la wananchi kuwa na mipango ya ardhi ni kuhamasisha kilimo endelevu ndani ya jamii,wananchi kuwa na ushiriki katika kusimamia sekta ya kilimo.

Fidelis alisema mpango wa matumizi bora ya ardhi utafanyika katika vijiji 30,kwa kushirikiana na halmashauri husika,wananchi watapimiwa ardhi yao na kuingizwa kwenye matumizi yanayotambulika ili kupunguza migogoroya ardhi.
                                        
Mama Sayota Singa akichangia mada katika mdahalo wa nini kifanyike kupunguza migogoro ya ardhi katika kijiji cha Mela Mvomero. 

No comments:

Post a Comment