Nyamunga alisema wimbo Nipo,anawaambia mashabiki wake bado
yupo kwenye game ya bongo Flovour baadaya kupotelea kwenye siasa kwa muda
mrefu,na kuwajulisha bado anafanya siasa na muziki kwa pamoja
“mashabiki wangu nipo,nimerudi kwenye game, karibuni sana kuniunga
mkono,na mimi sintowaangusha katika kazi zangu za muziki”Alisema Bazgar.
Alisema kuwa wimbo wa Nipo,ni wimbo wa tano katika nyimbo
zake aliwatoa,zilizotengenezewa katika studio za Dizz Power na Bamiza zote
kutoka mjini Morogoro.
Bazgar ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Dumila,alisema
kuwa katika muziki msanii anayemkubali ni Afande Sele na AY,hii ni kutokana na
utunzi wao wa mistari yenye kuelimisha jamii na kukubalika kwao ndani na nje ya
Tanzania.
Pia aliwataka wasanii waliopo kwenye tasnia ya muziki
wakumbuke kuwa muziki ni biashara, hivyo wanatakiwa kujiamini,kujituma kutengeneza kazi zinazokubalika ndani ya
jamii na zenye kuelimisha.
No comments:
Post a Comment