Monday, October 17, 2016

UVCCM,WAWEKEZAJI WEKEZENI MOROGORO.


UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi,Wilaya ya Morogoro mjini,umeiomba serikali kukaribisha wawekeza wengi kuwekeza ndani ya mkoa kutokana na kuwa na meneo ya wazi ya kutosha,na nguvu kazi za vijana kufanya kazi katika viwanda vitakavyojengwa.

Mwito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa umoja huo,Salum Mkolwe wakati wakiadhimisha kumbukumbu ya miaka 17 ya kifo cha baba wa Taifa,Mwalimu Nyerere,ambapo waliadhimisha kwa kufanya usafi katika eneo lao lilipo Tungi,pamoja na kufanya tamasha la michezo.

Mkolwe alisema katika mkoa wa morogoro kuna mashamba pori mengi,hivyo ni wakati wa serikali kukaribisha wawekezaji kuja kujenga viwanda,ambavyo vitainua uchumi wa mkoa,pamoja na vijana kupata ajira za kudumu na kuepuka utegemezi

Alisema katika kumkumbuka hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere wameamua kumuenzi kwa kufanya usafi katika eneo lao wanalomiki lilipo tungi ambalo litatumika kama kitenga uchumi chaumoja huo,pia kufanya michezo mbalimbali ikiwemo mpira miguu,kuvuta kamba na kuimbiza kuku.

“tudumishe usafi wa mazingira,kujenga afya bora,vijana tuwe mstari wa mbele katika kutunza mazingira,maendeleo yanapatikana sehemu salama yenye mazingira ya kuvutia.”Alisema.

Pia alisema lazima tudumishe amani iliyoachwa na Mwalimu,kukiwa na amani na utulivu,kutawakuwa na siasa safi,utawala bora unaokubalika na maendeleo yatapatikana,hivyo vijana kuwa mstari wa mbele katika kuitunza amani ya nchi.

Kwa upande wake,Katibu UVCCM,Wilaya ya Morogoro,Peter Kabwe aliwataka vijana kutumia muda wao kujenga chama na kukitumika,vijana ndio wenye nguvu,tusiwaachie wazee chama.

Pia alisema kila kijana mwanachama wa ccm kuwa mbalozi katika eneo analoishi kwa kusema mazuri ya chama,viongozi wa matawi ya vijana kwa kila kata kuwa mfano ndani ya jamii,pia kuongeza idadi ya wanachama,kuhakikisha kuna wanachama hai,na wanaolipa ada ili kuimarisha chama chao.


Vijana wa UVCCM,wakifanya usafi katika kiwanja chao wanachomiliki eneo la Tungi Manispaa ya Morooro.
Wanachama wa UVCCM,wakijadiliana jambo kabla ya kuanza usafi katika kiwanja chao,ikiwa ni ishara ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa,Mwalimu Nyerere.
                                              


No comments:

Post a Comment