Tuesday, September 13, 2016

WAFANYABIASHARA WA NYANYA WALIA NA BEI MOROGORO.

                                               

WAFANYABIASHARA wa soko la Mawenzi lililopo Manispaa ya Morogoro wamesema uuzaji wa bidhaa sokoni hapo umeshuka kwa kiwango kikubwa kulingana na misimu iliyopita huku wakifanya biashara bila kuona faida.

Wakizungumza na Jambo Leo,kwa wakati tafauti,Donatha Urio alisema kuwa soko limekuwa na watu wengi ila wanaofanya biashara ni wachache sana kutokana na bidhaa kuwa nyingi ila wanunuzi wachache kutokana na mzunguko wa hela kuwa mdogo sana.

“nakaa sokoni hapa toka saa moja asubuhi mpaka saa kumi mbili jioni,Napata shilingi elfu nane kwenye mauzo,wakati miezi miwili iliyopita nilikuwa apata shilingi elfu hamsini kwa siku”

Shukuru Leonad alisema kuwa tatizo kubwa ni mzunguko wa hela kuwa mdogo sana,kiasi kinachochangia bidhaa kushuka bei kila siku,na wanunuzi wananunua kiwango kidogo kutokana na fedha aliyonayo mfukoni tofauti na miaka mingine iliyopita.

“fungu la viazi linauzwa shilingi mia mbili kutoka elfu tatu,nyanya ndoo efu moja kutoka elfu ishirini,hii haijawahi kutokea katika soko letu na inatufanya tubadili biashara”Alisema.

Leonad alisema kuwa kuna baadhi ya wafanyabishara wanashindwa kuagiza mizigo mipya kutokana ya zamani ipo,na bidhaa nyingine hasa matunda na nyanya zinaoza kutokana na kulimwa kwa wingi na kukosa sehemu ya kuhifadhi kwa matumizi ya badae.

Alisema kuwa wafanyabiashara wengi wanaogopa kuweka fedha zao sokoni kutokana na hawapati faida yoyote,ila anaamini huuni msimu wa mpito kwao na ipo siku mzunguko wa fedha utabadilika na kuweza kufanya bishara kwa kiwango cha juu na kupata faida.


No comments:

Post a Comment