Tuesday, September 13, 2016

HAKUNA KUTOA ARDHI KWA WAWEKEZAJI WAKATI WANANCHI HAWANA ARDHI YA KUTOSHA.


                                                

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro,Kibena Kingo amesema hataruhusu mwekezaji yeyote kupewa ardhi katika wilaya hiyo ikiwa bado wananchi wanaupungufu wa ardhi kwa lengo la kupnguza migogoro ya ardhi.

Alisema hayo katika tamasha  la nne la jinsia ngazi ya Wilaya 2016 lenye lengo la kumkomboa mwanamke kuwa na haki ya kumiliki Ardhi,huduma bora za jami linalofanyika kata ya Mkambarani katika wilaya ya Morogoro,kuandaliwa na TGNP Mttandao kwa kushirkiana na shirika la Action Aid.

Kingo alisema kuwa wanawake wengi sehemu za vijijini hawajui thamani ya ardhi licha ya kuitumia katika kuzalisha kila siku,ni wakati sasa wa kila mwanamke kutafakari nafasi yake katika kumiliki ardhi.

“mimi mwanamke kwangu ni wapi,ukimiliki hata hatua 10 za ardhi hapo ndiko kwako na sio kuwaachia wanaume kumiliki ardhi na mwanamke unakuwa nyuma kila wakati”alisema Kingo.

Aliwataka TGNP mtandao na wadau wenginie kuendelea kutoa elimu ya umiliki wa ardhi hasa sehemu za vijijini kunakofanyika mikataba hewa,hii ni kutokana na wananchi wengi kuwa na uelewa mdogo juu ya sheria za kumili ardhi.

“wanawake msipojitokeza kumiliki ardhi mtakuwa watumwa ndani ya nchi,jitokezeni katika mikutano ya ugawaji wa ardhi inayofanyika kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na seriakali”Aliongeza.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kiloka,Robert Selasela alisema kuwa TGNP Mtandao imewasaidia sana kutoa elimu kwa wananchi wa kata yake hasa katika kujitambua na kujua haki zao za msingi na suala zima umuhimu wa kumiliki ardhi.

Selasela alisema changamoto nyingi zimeibuliwa na wadau hao katika maeneo mbalimbali,hivyo imewasaidia viongozi kupata matatizo ya wananchi wao kwa karibu sana na hata kabla ya kufanya ziara ndani ya kata zao.




No comments:

Post a Comment