MKUU Wa mkoa Wa Morogoro Dk Steven
Kebwe amezitaka halmashauri zote wilayani humo kuchukua hatua za haraka na
kurudishwa fedha zilizochukuliwa na watumishi hewa kwani muda uliotolewa wa
kukamilisha zoezi hilo umeisha.
Dkt.Kebwe alitoa agizo hilo katika kikao
cha siku mbili cha wajumbe wa ALAT mkoa Wa Morogoro kinachofanyika katika mji
Wa Ifakara wilayani Kilombero.
Dk Kebwe alisema kuwa halmashauri za
Wilaya katika mkoa huo zimekuwa kimya katika suala hilo kwani hadi hivi sasa ni
Wilaya moja tu ya Kilosa ndio iliyofanyia kazi suala hilo na kufikisha taarifa
yake katika ofisi ya Mkuu Wa mkoa.
Ameziagiza halmashauri zilizobaki
kujitazama upya na kuharakisha suala
hilo kwani Fedha hizo zikirudishwa zitakwenda katika masuala mbalimbali ya
wananchi ikiwemo kukamilisha madawati katika shule.
Alisema baada ya kuunda timu ya
kujiridhisha ili kufuatilia idadi ya watumishi hewa mkoani humo ilibainika kuwa
mkoa wa morogoro ulikuwa na watumishi hewa 315 ambao wameitia hasara serikali kiasi
cha shilingi bilioni 2.2.
Amebainisha kuwa hapo awali aliambiwa
mkoa una watumishi hewa 149 tu na yeye kuamua kujiridhisha na baadae kubaini kuwa
idadi aliyopewa mwanzo hata mara ya pili hazikuwa za kweli wowote.
Aidha Mkuu huyo amezitaka halmashauri
hizo kusimamia na kutenga fedha asilimia
10 zitakazokwenda kwa vikundi vya vijana na wanawake na pia kujidhatiti na kuhakikisha hakutokuwepo na migogoro ya Ardhi katika halmashauri zao.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo Wa
mkoa ameziagiza halmashauri hizo hadi mwisho wa mwezi huu ziwe zimepeleka mpango
mkakati a kuongeza mapato katika halmashauri zao.
Awali akimkaribisha mkuu wa
Mkoa,Mwenyekiti Wa Alat mkoa wa Morogoro Pascal Kihanga alisema lengo la kikao
hicho cha siku mbili ni kufanya maandalizi kimkoa kwa ajili ya kikao cha Alat
kitaifa kitakachofanyika Septemba 22 mwaka huu.
Kihanga alisema mafunzo hayo ni ya kuwajengea
uwezo wajumbe tokana na viongozi wapya
kuwa wageni na pia kuelewa masual ya ulinzi na Usalama na kujifunza mfumo Wa ukusanyaji wa
mapato kieletroniki kama serikali kuu ilivyoagiza.
No comments:
Post a Comment