Wednesday, July 13, 2016

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA WATAKIWA KUACHA SIASA KWENYE MIRADI YA MAENDELEO.

                                                  
Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini,Abdulazizi Abood akikabidhi mabomba ya kusambaza maji katika mtaa wa Magereza kata ya Kihonda Manispaa ya Kihonda.

VIONGOZI wa serikalia za mitaa na kata katika manispaa ya Morogoro wametakiwa kusimamia miradi ya maendeleo na kuweka siasa pembeni ili wananchi wa chini kuweza kufaidika na matunda ya serikali yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mbunge wa Morogoro mjini,Abdulaziz Abood wakati akikabidhi mabomba ya kupitisha maji katika Kata ya Kihonda mtaa wa Magereza ambapo alisema thamana ya miradi ya maendeleo ya serikali ipo mikononi mwa viongozi wa serikali za mitaa na  kata.

Alisema kuwa miradi yote lazima iwe inatembelewa na viongozi wa eneo husika na kuweza kuangalia mwenendo mzima na kuweza kutoa taarifa kwa viongozi wa juu endepo kuna tatizo ili kuweza kufanyiwa kazi na sio kuacha mpaka wananchi kuanza kulalamika na kuandamana.

Abooda alisema tatizo la maji katika manispaa ya mororgoro hususani kata ya Kihonda litamalizika kwania serikali imeshajipanga kushiriakiana na wafadhili na idara ya maji kuhakikisha wananchi wake hawapati shida ya maji safi na salama.

Aliwataka viongozi na wananchi wa mtaa wa magereza na jirani ambapo mabomba hayo yatasambazwa kwa ajili ya kusambaza maji katika maeneo yao kuwa walinzi na kuhakikisha yanakuwa katika mazingira salama kila mara.

Nao wakazi wa Mtaa wa Magereza kata ya Kihonda,walisema kuwa jitihada zinazofanywa na mbunge Abood na serikali zitasaidia kupunguza kero ya maji iliyokuwa inawatesa kwa kipindi  cha miaka mingi na kufanya kushindwa kufanya shughuli nyingine za uzalishaji na kutafuta maji.

                     



No comments:

Post a Comment