Tuesday, June 28, 2016

SMILE COMMUNICATION WAPIGA HODI MOROGORO.



Meya wa Manispaa ya Morogoro,Pascal Kihanga akikata utepe kufungua ofisi ya Kampuni ya Smile Communication mkoani Morogoro.
WAKAZI wa Manispaa ya Morogoro wametakiwa kutumia huduma zinazotolewa na  huduma za mawasiliano katika kupata taarifa mbalimbali ikiwemo za kibiashara ili kufanya shughuli zao kirahisi na ufanisi zaidi kwa lengo la kujipatia maendeleo.



Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro,Pascal Kihanga wakati akifungua Duka la Smile mjini Morogoro,ambapo alisema huduma hiyo ya mawasiliano itaaidia sana kuleta maendeleo ya watu binafsi na masnipaa kwa ujumla.


Kihanga alisema kuwa wakazi wa manispaa ya Morogoro sasa wataweza  kunufaika na huduma zinazotolewa na kampuni hiyo  na hivyo kuwaletea mapinduzi mapya ya kasi ya internet kupitia mitambo ya Smile 4G LTE .



Kihanga alisema kupitia huduma zinazotolewa na kampuni hiyo   itakuwa faraja kwa wananchi hususani wafanyakazi ,wafanyabiashara na kwa matumizi ya   nyumbani  wakiwemo wanafunzi  ambao wataweza kutumia huduma ya mtandao  utakaowarahisishia kutuma  na kupokea taarifa. .


‘’Sasa wafanyabiashara na hata wakulima wanaweza kunufaika na huduma za mtandao  uendao kasi katika kupata taarifa mbalimbali za masoko na hata kibenki.’’alisema.


Kwa upande wake Meneja wa Mkoa wa Morogoro na Dodoma wa Kampuni hiyo  Zephania  Mgonella alisema kuwa  katika sekta ya mawasiliano  hapa nchini Tanzania intaneti ya 4G LTE kwa sasa ndio  inayoongoza  kwa sasa kwa kuwa na kasi mara sita  zaidi kuliko 3G  na mara nne zaidi kuliko 3.75G.



Mgonella alisema  kuwa  kupitia teknolojia hii  wananchi wa Morogoro wana  uhakika wa kasi ya upakuaji na kasi ya upakiaji wa mafaili ,barua pepe,nyimbo na michezo ,matumizi  ya nyenzo mbalimbali  za kwenye mtandao  na kwa kuangalia  video  na televisheni  bila  kugomagoma.



Hata hivyo alisema kuwa Kampuni ya Smile ilianza rasmi mwaka 2012 na tayari imefungua matawi yake katika Mkoa wa Dodoma,Daressalaam,Mwanza ,Arusha ,Moshi,Mbeya  na hatimaye Morogoro kwa sasa.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Smile Communication,Zephania  Mgonella akitoa maelezo juu ya utendaji wa Kampuni hiyo kwa Meya wa Manispaa ya Morogoro,Pascal Kihanga katika ufunguzi wa ofisi ya mkoa wa Morogoro.
                  



No comments:

Post a Comment