Wednesday, June 22, 2016

KAYA 6931 ZAPATIWA MIL.240.5 KUTOKA TASAF.

JUMLA ya shilingi milioni 240.5 zimetolewa kwa Kaya 6931 katika Wilayani Gairo mkoani Morogoro kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) huku kaya 124 zikitolewa katika mpango huo kwa kukosa vigezo.

Mratibu wa TASAF,wilaya ya Gairo,Annajoyce  Rubagumisa alisema zozezi hilo limefanyika kwa awamu ya sita sasa,na walifanikiwa kutoa fedha kwa wale wote waliokidhi vigezo na 124 waliondolewa kutokana na kutokuwa na vigezo vilivyowekwa.

Alisema lengo la  kutoa hela ni kuziwezesha kaya maskini kuongeza kipato  na fursa za kuboresha upatikanaji wa mahitaji muhimu,na wanashirkiana na viongozi wa serikali za vijiji kuhakikisha ruzuku hizo zinakwenda kwenye matumizi sahihi.


Rubagumisa alisema jumla ya vijiji 50 vimepatiwa ruzuku hiyo,na kaya 124 ziliondolewa kutokana na kubainika kuwa na  uwezo wa kujitegemea katika maisha yao.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Chamkobwe kata ya Chagongwe,Gadson James alisema mpango huu wa serikali wa kuangalia kaya maskini unasaidia sana wananchi kuweza kujimudu kimaisha na wengine kuwekeza katika kilimo.

James alisema kaya zilizopatiwa ruzuku hiyo huwa wanawafuatilia kuangalia matumizi ya fedha hizo na kuona ziko katika matumizi sahihi na wengi wao wamebadilika kimaisha.


Nae Mkazi wa Chamkobwe,Happness Eliakimu,aliishukuru serikali kwa kubadili maisha ya familia zao,kwani wameweza kuwanunulia watoto sare za shule,kupeleka shamba,pia aliiomba serikali kuendelea kutoa ruzuku kwani kwa kufanya hivyo inajiimarisha kwa wananchi wake.
Mwisho.
Kijiji cha Chamkobwe kata ya Chagongwe wilayani Gairo wakisubiri kupewa ruzuku ya TASAF.
w

No comments:

Post a Comment