Friday, September 16, 2016

RC.MAAFISA LISHE TEKELEZENI MAJUKUMU YENU.

                                          
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Dkt.Steven Kebwe akiongea na maafisa lishe.
MKUU wa mkoa wa Morogoro,Dkt.Steven Kebwe amewataka maafisa lishe katika halmashauri kutoa elimu ya kutokomeza suala la lishe duni,sio kukaa maofisi na kuapangiwa kazi nyingine tofauti na mikataba yao ya kazi.

Dkt.Kebwe alisema hayo katika kikao cha kujadili na kuweka mikakati ya kupunguza lishe duni katika halmashauri za mkoa wa Morogoro,Pwani na Dar es salaam kilichoandaliwa na Partinership for Nutrition in Tanzania(PANITA) kanda ya Mashariki.

Alisema kuwa katika halmashauri kuna maafisa lishe,ila wamekaa tu maofisini badala yakuzunguza mitaani na kutoa elimu jinsi ya kumaliza lishe duni,wafanye kazi walizopangiwa sio kufanya kazi tofauti na mikataba yao ya ajira.

Dkt.Kebwe aliwataka maafisa lishe kuhakikisha kila mpango kazi katika halmashauri suala la lishe linaingizwa na kupewa kipao mbele,afya ni muhimu sana hivyo mtu haiwezi kuzalisha kama hana afya nzuri.

Kwa upande wake Mratibu wa Lishe Kanda ya Mashariki,Gaudencia Donati alisema kuwa lengo la kukutana ni kupeana uzoefu na kuweka mikakati ya kutokomeza lishe duni katika maeneo mbalimbali.

Donati alisema suala la lishe duni lazima lishughulikiwe na kila mtu,kuhakikisha watoto wanazaliwa na afya nzuri,wakina mama wajawazito wapewe elimu ya kutosha ili kuweza kujifungua watoto wenye afya nzuri.

Mganga wa Manispaa,Baraka Jonas alisema kuwa lishe duni inasababishwa na ukosefu wa protein,damu na madini joto,hivyo wadau wa afya washirikiane kuhakikisha virutubisho vinakuwepo katika vyakula mbalibmali wanavyotumia.

Jonas alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha wakina mama wanapata elimu wanapokwenda kliniki,na umuhimu wa kunyonyesha watoto wao pindi wanapojifungua ili kuweza kutokomeza lishe duni.



No comments:

Post a Comment