SERIKALI
imesema itaendeleza sera ya Kilimo Kwanza na kuhakikisha mkulima anaondokama na
kilimo cha jembo la mkono kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao
yatakayotumika katika viwanda vya hapa
nchini.
Kauli hiyo
ilitolewa Mwishini mwa wikia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Dr.Florens
Turuka katika uzinduzi wa mpango mpya wa Uashirikiano baina ya taasisi za umma
na binafsi kwa ajili ya kuendesha mafunzo bora ya zana za kilimo uliofanywa na
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.(SUA).
Dr.Turuka
alisema zana za kilimo bado zinahitaji
na hivyo ni wakati wa sekta binafsi kutumuia nafasi hiyo kuweza kumsaidia
mkulima na mjasiariamali kuweza kuzalisha kwa wingi ili sekta ya viwanda
inavyokuwa isikije kukosa mali ghali ama kutegemea kutoka nje.
Kwa upande
wake,Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA),Prof.Gerald Monela alisema SUA
wakishirikiana na mradi wa ubunifu katika utafiti wa kilimo (iIAGRI) na kampuni
ya zana za kilimo ya John Deer wamezindua mpango wa matumizi bora ya trekta na
utafiti.
Prof.Monela
alisema mpango huo unalengaa kutoa elimu ya vitendo kwa wakulima kwa minajili
ya kuongeza uzalishaji kwa njia bora ya zana za kilimo,elimu itakuwa inatolewa
kwa wakulima na wamiliki matrekta kutoka pande zote Tanzania.
Nae
Mkurugenzi wa mradi wa Ubunifu katika utafiti wa Kilimo,(iAGRI)Prof.David
Kraybill alisema mradi unalenga kuandaa kizazi kijacho cha viongozi wa kilimo
katika taasisi za umma na za binafsi na
kuimarisha taasisi mahususi za utafiti
na mafunzo ya kilimo nchini.
Kraybill
aliongeza kuwa mradi huo unaandaa wahadhiri,watafiti,maafisa ugani na wanafunzi
katika kuboresha mbinu za kutatua matatizo ya wakulima wadogo na wale
wanaofanya biashara kilimo.
No comments:
Post a Comment