Wednesday, April 6, 2016

KAMPENI YA MZEE KWANZA TOA KIPAUMBELE APATE HUDUMA YAZINDULIWA.

SEIKALI imeagiza halmashauri zote nchini kuwakati kadi za bima ya Afya wazee wote wenye umri kuanzia miaka 75,na kupatiwa huduma ya vipimo vya magonjwa yote bure pamoja na kuhimiza kutenga dawati maalumu la kuhudimia wazee

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto,Ummy Mwalimu katika uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa Mzee Kwanza Toa Kipaumbele apate Huduma iliyofanyika mkoani Morogoro.

Sambamba na hilo,Waziri Ummy ameuagiza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuwalipia wazee 50 kwa kila  Halmashauri nchini kuweza kupata kadi za bima ambazo wataweza kuzitumia katika kuapata huduma za afya katika vituo vya afya na zahanati.

Mwalimu alisema lengo la kampeni hiyo ni kuikumbusha jamii ya watanzania kuhusu wajibu wa kuwapa wazee hadhi wanayostahili katika maeneo mbalimbali ya huduma za kajamii.

Alisema serikali kupitia wizara ya Afya imeandaa muswaada wa kutungwa kwa sheria ya wazee ambayo itapelekwa bungeni ili ipitishwe kuwa sheria ambayo itasimamia upatikanaji wa haki na ustawi wa sheria ya wazee.

Pia alizitaka halmashauri zote kubaini wazee walio katika maeneo yoa na kuhakikisha wanapata huduma zote za msingi ikiwa ni pamoja na huduma za afya kutoka kwenye mapato yao wenyewe na viongozi wote wa halmsahuri kusimamia zoezi hilo kwa ufanisi mkubwa.
                                   

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF),Michael Mhando alisema kuwa mfuko umetambua mchango mkubwa wa wazee katika taifa,na wanaungana na serikali kuhakikisha wanapata huduma bora muda wote.

Mhando alisema toka kuanzishwa kwa mfuko huo mwaka 2007 wamekuwa wakitoa huduma kwa wazee kupitia kadi za bima,na wanaendelea kweka mazingira mazuri katika kuhakikisha wazee wote wanahudumiwa vizuri katika sekta ya Afya.

Naye Mwakilishi wa Taasisi ya Help Age International,Danie Smart alisema hakuna nchi inaweza kuendelea bila kujali wake hususani wazee,hivyo jambo linalofanywa na NHIF na serikali kuzindua kampeni ya kuwaseme wazee linapaswa kuungwa mkono na watanzania wote.

Smart alisema katika tafiri zilizofanyika hivi karibuni katika masula bora ya Afya iliyoshirikisha nchi 96,Afrika kulikuwa na nchi 11 na Tanzania imeshika nafasi ya 2 katika kutoa huduma bora za kiafya kwa wananchi wake,na nafasi ya kwanza ikishilikiliwa na Mouritoius.



No comments:

Post a Comment