Sunday, April 24, 2016

Mbunge wa Morogoro mjni,Aziz Abood afanya ziara shule ya msingi Lugala iliyoanguka.

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro mjini,Abduaziz Abood amesema atatengeneza darasa moja katika shule ya msingi Lugala iliyopo kata ya Mindu baada ya wanafunzi kukaa kwa mwezi mmoja kwa kukosa darasa kutokana na shule hiyo kuanguka.

Akizungumza na wakazi wa mtaa wa Lugala na wanafunzi,Abood alisema ili wanafunzi waendelee kupata elimu na kuachaku kaa nyumbani atatengeneza darasa moja ambalo litatumika kusomea huku wakisubiri taratibu nyingine kutoka kwa tume iliyoundwa manispaa kufanya uchunguzi wa tukio hilo.

Abood alisema mkandarasi aliyesimamia ujenzi wa shule hiyo lazima ahojiwe  na timu yake yote kutokana na ujenzi kuonekana haukuwa imara na haukufuata vigezo vinavyotakiwa ndio maana shule hiyo ilianguka na kusababisha hasara kubwa.

Pia aliwataka wakazi wa mtaa wa Lugala iliyopo shule hiyo kufanya usafi katika mazingira yanayozunguka shule hiyo ili wanafunzi kuweza kusoma katika mazingira salama,na kujitolea katika shughuli za maendeleo ya ukarabati shule hiyo pamoja na kuhakikisha matundu ya choo yanakuwa salama kwa watoto.
Kwa upande wake Mwalimu wa shule hiyo,Antony Shayo alisema kuwa anashukuru jitihada za mbunge za kujitolea kutengeneza darasa hilo,pia watoto waliokuwa wanakaa chini ila mbunge alijitolea madawati 40,kutokana na shule kuanguka walikosa sehemu ya kuweka ila darasa likikamilika wanaamini watapata madawati hayo.
Shayo alisema kuwa shule hiyo ilianza februari 2016,ina jumla ya wanafunzi 85,huku ikiwa na walimu wawili wanaojitolea kufundisha,na darasa likikamilika itabidi waongeze muda wa ziada wa wanafunzi ili kuendana na mtaala.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Lugala,Sanga Mkulago alisema kuwa waliohusika katika kusimamia ujenzi wa shule hiyo wakiongozwa na mtendaji kata hawafai,na watakaobainika kurubuni mradi huo wachukuliwe hatua za kisheria kwani kuhamishiwa mtaa mwingine wataharibu kama walivyofanya Lugala.      
                                 
Mbunge wa Morogoro mjini,Aziz Abood akiongea na wananchi na wanafunzi wa shule ya msingi Lugala iliyoanguka na wanafunzi kukosa sehemu ya kusomea.

Mbunge wa Morogoro mjini,Aziz Abood akikagua jengo la shule ya msingi Lugala iliyopo kata ya Mindu  iliyoanguka kutokana na ujenzi wake kuwa hafifu.

No comments:

Post a Comment