Thursday, March 17, 2016

Kampuni ya M-Power yazindua ofisi Mkoa wa Pwani katika kata ya Mkuza.

                                                               
Meneja wa Kampuni ya M-Power mkoa wa Pwani Adamu Ndimbo akiwakaribisha wageni katika hafla ya ufunguzi wa ofisi ya M-Power
Mrakibu wa Polisi  Mkoa wa Pwani.Bakari Kawinga akipata maelezo ya kampuni ya M-Power inayosambaza umeme wa jua kutoka kwa viongozi wa M-Power kabla ya ufunguzi wa ofisi ya mkoa wa Pwani.

Baadhi ya wafanyakazi wa Kamupni ya M-Power wakiburudika katika hafla ya uzinduzi wa ofisi ya mkoa wa Pwani.


Meneja wa Usambazaji wa Kampuni ya M-Power Tanzania,Alfred Kohi akizungumza na wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa ofisi ya Mkoa wa Pwani.

Mkazi wa Kata ya Mkuza,Salum Rajabu akitoa ushuhuda baada ya kufungiwa umeme wa solar kutoka kampuni ya M-Power

Mtendaji wa Kata ya Mkuza,Adofu Masawa akiwakaribisha wageni ndani ya kata yake.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani,Evarist Ndikilo akizungumza na wakazi wa kata ya Mkuza na wafanyakazi wa Kampuni ya M-Power  katika hafla ya uzinduzi wa ofisi ya kampuni hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Pwani,Evarist Ndikilo na Meneja wa Usambazaji wa Kampuni ya M-Power Alfred Kohi wakikata keki kwa  ishara ya upendo katika ufunguzi wa ofisi ya Kampuni ya M-Power mkoa wa Pwani.

SERIKALI imesema itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wanaowekeza katika sekta ya umeme hapa nchini ili wananchi wake hasa wanaoishi maeneo ya vijijini kuweza kupata nishati hiyo na kupata huduma bora kwa wakati wote.


Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani,Evarist Ndikilo wakati akifungua ofisi za Kampuni ya M-Power inayosambaza umeme wa jua katika kata ya Mkuza,ambapo alisema serikali inaunga mkono wawekezaji wote wanaowekeza katika  kusambaza nishati ya umeme.


Alisema serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wote wanaoishi vijini wanapata nishati ya umeme,na hasa maeneo ambayo tanesco haijafika wanakaribisha wadau wa umeme kujitokeza kwa wingi kuweza kusambaza nishati hiyo.


Kwa upande wake,Meneja wa Usambazi wa Kampuni ya M-Power,Alfred Kohi alisema kuwa kampuni hiyo ilianza iina miaka 4 hapa nchini na hivi sasa wameshafikia wateja zaidi ya 100,000 katika mikoa 14 ambapo tayari wameshafungua ofisi na kuanza kazi ya usambazaji wa umeme wa jua.


Kohi alisema lengo la usambaza umeme wa jua ni kuhakikisha wananchi wa maeneo ya vijijini na mijini wanaotumia mafuta ya taa kuweka kwenye kibatari kuondokana na adha hiyo na kuweza kutumia umeme wa bei rahisi unaosambazwa na kampuni hiyo

Alisema kuwa kampuni imejipanga na kuhakikisha mpaka kufikia 2017 wanakuwa na wateja zaidi ya milioni 1 nchi nzima na kuhakikisha wananchi wa pembezoni mwa miji wanaondokana na matumizi ya mafutaya taa ambayo yanasababisha magonjwa ya macho na kukuhoa kutokana na moshi wa kibatari.


Pia alisema wanatoa huduma kwa vituo vya afya na vituo vya polisi vilivyo pembezoni mwa mji ambavyo havijafikiwa na nishati ya umeme wa tanesco kwa kuvifungia mtambo wa umeme wa jua bure ikiwa ni kutambua umuhimu wa huduma zinazotolewa na vituo hivyo kwa wananchi


Nae mkazi wa kata ya Mkuza,Salum Rajabu alisema kuwa huduma iyosambazwa kamapuni ya M-Power ni bei nafuu na wananchi wa kipato cha chini anaweza kumudu na kuomba seriakali na wadau wengine kuwaunga mkono pindi wanapofika katika maeneo yao kutoa huduma.


No comments:

Post a Comment