Tuesday, December 15, 2015

WANANCHI WA KIJIJI CHA MINDU MANISPAA YA MOROGORO WAUAKANA UONGOZI WA SERIKALI KIJIJI HICHO

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro,Mihungo Ruyemamu akiangalia risiti zilizotumika kuweka fedha benki katika akaunti ya kijiji cha mindu

Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Morogoro wakitembelea mgodi wa kuchimba mchanga katika kata ya Mindu.

Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini Aziz Abood akiongea na wananchi wa Kata ya Mindu.


WANANCHI wa Kijiji cha Mindu Kata ya Mindu Manispaa ya Morogoro wameiomba serikali ya Wilaya kubadili uongozi wa serikali ya kijiji kutokana na utendaji mbovu wa viongozi hao pamoja kutoa kauli chafu kwao pindi wanapodai haki zao za msingi.
Wakizungumza katika kikao kilichojumuisha kamati ya Ulinzi na Usalama ya Morogoro,Said Mkmba alisema kuwa watendaji hao wa kijiji wamekuwa wakiitisha mkutano na kusoma mapato na matumizi ya fedha zikiwa hazijakamilika na hivyo kuzuka kutokuelewana na viongozi hao kwa muda mrefu.
 “Tunaomba waondoeni viongozi hawa wa vijiji,hawatufai kabisa kutokana na utendaji wao pamoja na kutoa lugha za matusi na vitisho kwa wananchi wanaodai haki zao hasa upande wa matumizi ya fedha za miradi ikiwemo uchimbaji wa mchanga”Alisema Mkamba.
 Zainabu Abdallah alisema kuwa mradi wanaoutegemea katika pato la kijiji ni mradi wa uchimbaji wa mchanga ambao wamewapa waekezaji wa ndani ila kinachosikitisha ni matumizi na mapoto ya ushuru uliotozwa wawekezaji hauleweki unaenda wapi.
Kwaupande wake Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini,Abdulaziz Abood  aliungana na wanachi hao na kusema kuwa uongozi huo unapaswa kubadilishwa kutokana na kulalamikiwa mara kwa mara na wananchi katika utendaji wao mbovu
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro,Mihungo Ruyemamu alimtaka mkurugenzi wa Manispaa kumuondoa mtendaji wa kijiji cha Mindu,na kufanya hivyo ni pamoja kulinda usalama wake kutokana na wananchi kutokuwa na imani nae kabisa.
Ruyemamu pia alimtaka mkurugenzi huyo kushirikiana na kamati ya mazingira kuhakikisha eneo la mgodi wa mchanga linakuwa na vyoo ili kuepuka magonjwa ya mlipuko kutokana na wanachi wanaochimba mchanga wanajisadia vichakani kwa muda mrefu.
Hata hivyo aliwataka viongozi wa kijiji hicho kupeleka muhtasari za vikao,taarifa ya fedha ofisini kwake ili kufanyiwa ukaguzi na wakaguzi wa ndani wa manispaa na kuahidi kutoa taarifa ya ripoti hizo kwa wananchi hao pindi zitakapokamilika.
Nae Mtendaji wa kijiji cha Mindu,Yusufu Ahmed alisema kuwa wamekuwa wakiitisha mikutano ya kijiji lakini wananchi hawajitokezi hivyo kushindwa kujua miradi ya maendeleo ndani ya kijiji inaesndeshwa aje na ipo katika hali gani.
Mnamo tarehe 10/12 wananchi zaidi ya 30 kutoka kijiji cha mindu waliandamana hadi ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini Aziz Abood wakidai kuondolewa kwa uongozi wa kijiji waliowatuhumu kwa kuuza maeneo hovyo,ushuru wa mchanga na kutosomewamapato na matumizi.
Mwisho.


No comments:

Post a Comment