Tuesday, December 1, 2015

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUFUKUZWA SHULENI.

SERIKALI mkoani Morogoro imewataka walimu wa shule za msingi kuacha tabia ya kuwafaukuza wanafunzi wanaokosa baadhi ya vifaa na sare za shue kwani  jukumu la kuwanunulia vifaa hivyo ni wazazi na walezi na kuendelea kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero,Betty Mkwasa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoawa Morogoro,Dkt.Rajabu Rutengwe katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizoandaliwa na Kituo cha Wasaidizi wa Sheria pamoja na Dawati la Kijinsia kutoka kituo cha Polisi kwa udhamini wa WILDAF.

Mkwasa alisema jukumu la kuhakikisha watoto wanasoma na kupata elimu bora ni wazazi na walimu,hivyo ni jambo la aibu kuona mwalimu anamfukuza mtoto shuleni kwenda kwa kukosa vifaa ama sare za shule badala ya kuwasiliana na wazazi wake kujua taitozo liko wapi huku mwanafunzi akiendelea kusoma

Alisema imefikia wakati sasa jamii kuondokana na dhana potofu ya kumsomesha mtoto wa kiume na kumwacha wa kike,hii imepitwa na wakati kwani watoto wote wana haki sawa ya elimu na serikali ya sasa itahakikisha watoto wote wanasoma bure bila kusumbuliwa mashuleni

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Wasaidizi wa Sheria,Flora Masoy alisema takwimu zinaonesha kwa kipindi cha mwaka 2015 kesi za ukatili wa kijinsia zilizoripotiwa katika kituo chao zilikuwa 158,ambapo watoto 38 wakiume na 120 watoto wa kike waliofanyiwa ukatili tofauti.

Masoy alisema amoja na jitihada zinazofanywa zinazofanywa na serikali, vitendo vya ukatili wa kijinsia bado vinakithiri katika jamii zetu,hivyo sababu za makusudi zinatakiwa   kuhamasisha  jamii kushiriki kikamilifu katika kuzuia ukatili wa Kijinsia kwani kwa kiasi kikubwa jamii imekuwa ikichochea au ikikubali uwepo wa ukatili wa kijinsia kwa kutokutoa taarifa  au kuchukua hatua  kukemea ukatili wa kijinsia.

Aidha aliiomba serikali kuchukua  hatua za makusudi kurekebisha Sheria zinazohamasisha ukatili wa kijinsia,sababu zote zinazochangia watoto kukosa haki ya elimu pamoja na kutungwa kwa  Sheria   ya  ukatili wa kijinsia na  adhabu kali zitolewe kwa watu wanaohusika na ukatili wa kijinsia hasa wanaokatisha wanafunzi masomo.
Mwisho.

Wananchi wa Manispaa ya Morogoro,wakiwa katika maandamano ya kuadhiisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia dunia.

Mkurugenzi wa Kituo cha Wasaidizi wa Kisheria,Flora Masoy akisoma risala katika maadhimisho  ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoani Morogoro zilizofanyika katika viwanja vya mashujaa.

No comments:

Post a Comment