Tuesday, October 23, 2012

NMB YAOKOA WANAFUNZI 2I6 WILAYANI KILOSA KUKAA CHINI MADARASANI

                                                           
                                         Meneja  wa NMB kanda ya Mashariki Bw Gabriel Ole Loibanguti
                                         akimkabidhi msaada wa madawati Mwl mkuu  wa shule ya msingi
                                          ya Mvumi wilayani  Kilosa  mkoani Morogoro .
                                       
Kilosa .
Jumla  ya watoto 216  katika  shule  ya msingi  ya  Mvumi wilayani Kilosa mkoani Morogoro wameondolewa  adha  ya  kukalia mikeka  na mawe  wakiwa  darasani  kufuatia benki  ya NMB mkoani Morogoro kutoa msaada  wa madawati 85 na  meza tano  vitu  vyote  vikiwa  na tahamni  ya  shilingi mil 5.
Akiongea na waandishi  wa habari jana katika  hafla  hiyo   fupi ,afisa  utumishi wa halmashauri  ya wilaya  ya Kilosa Bw Ayoub Kambi kwa  niaba ya mkurugenzi wa halmashauri  hiyo alisema  kuwa benki  hiyo imekuwa msaada  mkubwa  katika kutatua  kero mbalimbali zinzoikabili  sekta  ya  elimu .
Bw  kambi   alisema kuwa   wilaya  ya Kilosa  imekuwa na changamoto mbalimbali  katika  sekta  ya  elimu lakini  taasisi  hiyo  ya  fedha  ya NMB  imekuwa  mkombozi  mkubwa  katika  kuzitatua kero  hizo kwa  kiasi  kikubwa .
“Ni kweli watoto  wengi wanakaa  chini madarasani hali ambayo inawafanya wanashindwa  kufanya  vizuri kimasomo darasani kutokana na kusoma  katika mazingira mabaya “alisema Bw  kambi

Alisema  kuwa  ni wazi maombi  ya  misaada  katika   taasisi  hiyo  yamekuwa  mengi  kutoka  maeneo mbalimbali  ya kanda  ya mashariki , lakini  wilaya  ya kilosa  imekuwa na bahati  katika  kufanikisha maombi  yao .

Aidha  alisema  kuwa kwa kiasi    kikubwa  benki  hiyo imekuwa ikisaidia  kupunguza mzigo wa halmashauri na  wazazi  katika  kutatua  changamoto zilizopo  katika  sekta  ya elimu  .

Alisema  kuwa  benki  hiyo imekuwa mstari wa mbele  katika  kusaidia  misaada  mbalimbali  katika shule  za msingi na sekondari  hivyo  kwa niaba  ya wakazi katika wilaya  ya Kilosa na halmashauri  yake  hana budi  kuishukuru NMB .

Aidha  naye  meneja  wa NMB kanda  ya mashariki  Bw  Gabriel Ole Loibanguti  akizungumza  katika hafla  hiyo  ya kukabidhi madawati  hayo  na meza  kwa  mbele  ya kamati  ya  wazazi na  uongozi wa  shule   ya msingi Mvumi  aliwataka  wazazi kuhakikisha  wanaendeleza  watoto  kielimu .

Alisema  kuwa benki  ya NMB  kwa  kutambua  umuhimu wa elimu  kwa watoto  ndio mana  imekuwa mstari wa  mbele  katika  kuchanga  shughuli  za maendeleo ya  sekta  ya elimu na sio  kuchangia  shughuli za hanasa .

Aidha  katika hatua  nyingine  Bw Loibanguti aliwataka wazazi kuacha  tabia  ya kuchangia   zaidi  shughuli za  hanasa  kama ngoma , unyago , kitchen part na harusi  na badala  yake  kujenga  tabia  ya kuwawekea  watoto  akiba  kwa ajili  ya  kuwaendeleza  kielimu .

Alisema kuwa  NMB  inayo  huduma  ya  akaunti  ya watoto  maarufu  kwa jina  na Junior akaunti  imekuwa njia  sahihi  ya  kumfanya mtoto  kusoma   shule  bila  ya kuwa na wasiwasi  wa kukatisha masomo kutokana na uhaba  wa  pesa .

Aidha  meneja   huyo wa kanda  ya mashariki  wa NMB  aliwataka  wazazi  shuleni hapo kuhakikisha kila mtoto anafunguliwa  akauti  ya Junior ili kumfanya mtoto asome  akiwa huru  bila  ya wasiwasi .
.

No comments:

Post a Comment