SERIKALI ya awamu
ya tano imeshauriwa kuhakikisha inaweka mfumo mzuri zaidi wa kusimimamia
sekta ya
madini hapa
nchini ili
kuweza kupiga hatua zaidi kimaendeleo na kukuza uchumi wake kama ilivyo nchi ya Afrika ya kusini .
Ushauri huo umetolewa jana na
Mtaalamu wa
madini ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya MTL Consulting ambayo
inajishughulisha na ushauri
wa sekta ya madini nchini John Tindyebwa wakati akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya ulewa juu ya masuala ya madini na sheria yake ya mwaka 2010 kifungu namba 4.
Tindyebwa alisema kuwa mafunzo
hayo yanatolewa kwa Waandishi wa habari wa Mkoa wa Morogoro yana lengo
la kuwapa ulewa juu ya mradi mpya wa Kampuni
ya Kibaran resources
Limited inayochimba madini ya
Kinywe (Graphite) katika machimbo Epanko Mahenge yaliyopo wilayani Ulanga mkoa Morogoro.
Alisema kuwa ni vyema serikali ya awamu ya tano ikahakikisha inaweka
mfumo mzuri zaidi utakaosaidia kuinua sekta ya madini kama zilivyo nchi nyingine mfano nchi ya nchi Afrika kusini ambapo imeonekana kupata mafanikio
makubwa kutokana na
kuweka mipango na
mikakati mbalimbali katika suala
zima katika sekta ya madini.
‘’Tunaishauri serikali ya awamu
ya tano ikaweka mfumo mzuri zaidi katika usimamizi wa sekta ya madini ili watanzania waweze kunufaika na rasilimali ya madini na
kukuza uchumi ‘’alisema .
.
Alitolea mfano mji wa
Johannesburg uliopo nchini Afrika ya Kusini kipindi
cha mwaka 1890 ulikuwa masikini lakini baada ya kipindi kifupi kugundulika
kuwa madini
na nchi kuweza
kuweka mfumo mzuri wa usimamizi wa madini yake nchi imeweza kukua kiuchumi na hata kujengekea na kuwa miongoni
mwa miji mikubwa duniani ambao umekuwa kwa kasi kutokana na sekta ya madini.
Pia alibainisha kuwa nchi ya Tanzania sio nchi masikini kwani imejaliwa kuwa na
rasimili kubwa ya madini ya aina mbalimbali lakini imeshindwa kuyatumia
kutokana na kutokuwepo na mfumo mzuri zaidi wa usimamizi wa rasilimali hiyo.
Kwa upande wao wanahabari
wakichangia mada inayohusu
sekta ya madini na uanzishwaji wa migodi Joseph
Malembeka na Nickson Mkilanya walisema
kuna haja ya serikali kuwatumia
wataalamu wa jiolojia katika kubaini maeneo yaliyo na uwezekano wa upatikanaji
wa madini ili kuweza kutambulika na kuepuka adha ya kuwahamisha wananchi
kiholela.
Hata hivyo waliishauri serikali kuweka sheria na mikataba ya wazi kwa wawekezaji itakayosaidia wananchi kunufaika na sekta ya madini hapa nchini
kutokana na mali hizo kupatikana ndani ya ardhi ya Watanzania
Mwishho.
No comments:
Post a Comment