WANANWAKE katika Wilaya ya Morogoro Tarafa ya Matombo mkoani
Morogoro wamesema rushwa ndio inachangia kwa kiasi kikubwa kushindwa kushiriki
katika chaguzi mbalimbali zinazofanyika kila nchini kutokana na hali zao za
uchumi kuwa duni
Hayo yalisemwa katika mdahalo wa Wanawake na Uchaguzi ulioandaliwa
na Kituo cha Msaada wa Wasaidizi wa Kisheria (MPLC) kwa ufadhili wa OXFAM Tanzania
katika program ya Fahamu Ongea sikilizwa iliyoshirikisha wanawake kutoka kata
za Konde,Mkuyuni,Kiloka,Mkamba na Kisemo katika Tarafa ya Matombo
Geniveva Peter na Zuhura Mfalme walisema kuwa katika kipindi cha
uchaguzi rushwa inatawala hasa ukikuta mwanamke ni miongoni mwa wagombea
anajikuta anashindwa siku zote kutokana na mpinzani wake kuwa na kipato cha juu
na kuweza kuwapa wapiga kura ili wampatie ushindi
“viongozi hivi sasa kwa asilimia kubwa wanapatikana kwa kutoa
rushwa,hivyo wanawake tunapaswa kubadilika na kufanya maamuzi ya kuwachagua viongozi
bora na sio wanaotokana na rushwa za fedha na vitenge ambao wakipata uongozi
wanajali maslahi yao”Walisema
Kwa upande wake Afisa wa Haki na Jinsia kutoka OXFARM Tanzania,Rashida Shariff alisema
katika program ya Fahamu Ongea Sikilizwa lengo lake ni kuhamasisha
wanawake na vijana kushiriki katika
uchaguzi mkuu,na kupatiwa elimu ya uchaguzi huru na haki ili kuweza kupata
fursa ya kutambua kiongozi gani anafaa kuongozi jamii
Rashida alisema wanawake wamekuwa wakidhalilishwa sana kipindi cha
uchaguzi kwa matusi,na kashfa na wamekuwa wakitumiwa sana kama madaraja ya
rushwa na wagombea na kujisahau kama wao ni waathirika wakubwa pindi watakapomchagua
kiongozi ambaye hatawajali na kujali maslahi binafsi
Aliwataka wanawake wasikubali kuwa watumwa wa rushwa katika
kipindi cha uchaguzi,kutokubali kushurutishwa na wanaume kupiga kura kwa
kiongozi ambaye hampendi,na kutunza vitambulisho vya kupiga kura ili visije
kuibiwa na kufichwa na wapenzi wao ama marafiki wenye kumpenda mgombea fulani
kwa maslahi binafsi
Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Wasaidizi wa Kisheria,Flora
Masoyi,aliwataka wanawake kutambua kuwa kura ni siri,pia kutambua matatizo ya
wanawake ni mengi na hayana chama,hivyo ni wakati wa kuchagua kiongozi bora
ambaye ataweza kupambana na changamoto zinazowakabili wanawake nchini
Mwisho.
No comments:
Post a Comment