Monday, August 19, 2013

PONDA APANDISHWA KIZIMBANI KUSOMEWA MASHITAKA

                                                              
                                                                     
Ponda akiwa chini ya ulinzi wa polisi akipelekwa katika mahakama ya hakimu mkazi mfadhiwa wa mkoa wa morogoro kujibu mashitaka yaliyokuwa yanamkabili.

Ponda akitoka mahakamani baada ya kusomewa mashitaka matatu yaliyokuwa yanamkabili na kukana yote,kurudihswa gerezani hadi Augusti 28.kesi itakapoendelea.
Askari wakiweka ulinzi mkali mara baada ya mahakama kumalizika na wakiwa tayari kumrudisha Ponda katika viwanja vya gofu kupandihswa kwenye hedikopta na kurudishwa Dar es salaam.

ULINZI mkali uliimarishwa katika maeneo ya manspaa ya Morogoro wakati Katibu  wa taasisi na Jumuiya za Kiislam Tanzania Shekhe Ponda Issa Ponda mkazi wa Dar es salaam jana alipofikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa Morogoro kujibu shitaka linalomkabili huku akiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi wakiwa na mbwa  baada ya kuwasili kwa herikopta ya jeshi la Polisi katika uwanja wa Gofu mjini Morogoro.

Wakili wa Serikali,Bernard Kongola alikisoma  mashitaka matatu  dhidi ya Shekhe Ponda Issa Ponda  mbele ya hakimu mkazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro Richard Kabate ,alisema mnamo Agosti 10 mwaka huu katika eneo la Kiwanja cha Ndege  manispaa ya Morogoro Ponda Issa Ponda aliwaambia “ndugu waislamu msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bwakwata ambao ni vibaraka wa CCM na serikali na kama  watajitokeza kwenu watu hao na watajitambulisha kwamba wao ni kamati za ulinzi  na usalama za misikiti,fungeni milango na madirisha ya msikiti yenu na muwapige sana”

Kongola aliimbia mahakama kauli ambayo ilikuwa ikiumiza imani za watu wengine,na kwamba hatua hiyo ni kinyume cha agizo la mahakama  ya hakimu mkazi Kisutu  Dar-es-salaam iliyotolewa na hakimu V. Nongwa  tarehe mei 9 mwaka huu ambayo ilimtaka ndani ya mwaka mzima kuhubiri amani, ambayo ni kinyume na kifungu cha sheria namba 124 cha mwaka 2002, shitaka ambalo alikana.

                                               
Ponda akishuka kwenye gari nje ya makahama.


Katika shitaka la Pilli,mshitakiwa, Agosti 10 mwaka huu katika eneo la Kiwanja cha Ndege manispaa ya Morogoro na mkoa wa Morogoro waliwaambia waislam serikali ilipeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala vurugu iliyotokana  na gesi kwa kuwaua,kuwabaka, na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni waislamu lakini serikali haikufanya hivyo kwa wananchi wa Loliondo walipokataa ,mwarabu asipatiwe kipande cha ardhi ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni wakristu  na kusema kuwa  maneno ambayo yaliumiza imani za watu wengine  ambalo ni kinyume cha kifungu cha sheria 129 cha mwaka 2002shitaka ambalo pia mashtakiwa  Ponda Isa Ponda  alikana.

Shitaka la tatu ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria mkuu wa serikali  Bernard Kongola kuwa mnamo agosto 10 mwaka huu eneo la kiwanja cha ndege manispaa na mkoa wa Morogoro mashitakiwa aliwashawishi waislamu kuwa serikali ilipeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu uliyotokana na gesi kwa kuwaua,kuwabaka na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni waislamu lakini serikali haifanya hivyo kwa wananchi wa Liliondo walipotaka Mwarabu asipatiwe kipande cha ardhi  ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao  kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni wakristo”

Wakili upande wa serikali alisema kuwa  maneno ambayo yalikuwa yakiumiza imani za watu  wengine na kwamba kufanya hivyo ni kinyume cha kifungu cha sheria  namba  390 na kanuni ya adhabu namba 35 cha mwaka 2002,  shitaka ambalo pia nalo Shekhe POnda Issa Ponda alikana.

Kwa upande wa utetezi,Ponda alikuwa akitetetewa na wakili Ignas Pungu na Bantalomeo Tarimo,huku upande wa serikali walikuwa wanaongozwa na Benedict Kongola,Gloria Rwakibalila, Asnab Mhando

Shekhe Ponda Issa Ponda aliwasilishwa kwa hedikopta ya jeshi la polisi katika uwanja wa Gofu mjini morogoro akiwa chini ya ulinzi wa polisi na kupandishwa katika gari maalum ambalo liliongozana na magari mengine matatu ya polisi huku ulinzi ukiwa umeimalishwa katika eneo la mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro wakiwemo askari wa Kikosi cha Kutuliza ghasia ,wa  upelelezi usalama wa taifa pamoja na mbwa wa jeshi la polisi wakati shughuli za kazi katika mahamaka hiyo na ofisi za jirani zikiwa zimesimama kwa muda.

Alifikishwa uwanja wa mahakama  majira ya saa 5.00 kamili asubuhi magari yalisimama kwa takribani  dakika 30 ndipo askari walishuka kwenye gari na kumfungulia mlango kisha kushuka na kuongozwa kwenye mahakama ya wazi ya hakimu mkazi mfawidhi  mkoa wa Morogoro huku umati wa wananchi ukiwa umefurika mahakamani hapo na kushuhudia kilichokuwa kinaendelea

Baada ya Kusomwa kwa mashtaka yote matatu wakili wa serikali aliiambia mahakama kuwa upelelezi wa kesi umekamilika na kupanga kesi kuanza kusikilizwa septemba 2 mwaka huu ambapo kwa upande wa utetezi uliomba mahakama kupanga kuanza kusikilizwa kwa kesi agosti 26 mwaka huu hali ambayo ilimlazimu hakimu Kabate kuwapa muda wa kujadiliana ambapo walitumia dakika tano kujadiliana na kurejea mahakamani na kupanga kuanza kusikilizwa kesi agosti 28 mwaka huu.
Mawakili wa upande wa utetezi walisema sababu za kuomba terehe hiyo ya kusikilizwa kwa kesi kwa kile walichoeleza kuwa mteja wao bado ni mgonjwa na anahitaji kupatiwa matibabu ya mara kwa mara hivyo anahitaji uangalizi

Hata hivyo mahakama ilipomalizika hali ya ulinzi iliendelea kuimarishwa na kupandishwa kwenye gari maalum alilopanda na kuelekea kwenye uwanja wa Gofu majira ya saa sita mchana  na kupandishwa kwenye hedikopta kwa ajili ya kurejeshwa gerezani  jijini Dar-es-salaam.

No comments:

Post a Comment