Wednesday, August 21, 2013

BENKI YA CRDB,CHUO KIKUU MZUMBE WATOA ZAWADI YA BAJAJI KWA MWANAFUNZI MLEMAVU



                                                     
Mwanafunzi mlemavu wa miguu,Salum Mnagwe akifurahi baada ya kukabidhiwa bajaji.

Mwakilishi wa Benki ya CRBD,Issa Singano akimkabidhi Salum nakala za pikipiki.
Makamu Mkuu wa chuo cha Mzumbe Prof.Joseph Kuzilwa akimkabidhi ufunguo wa bajaji mwanafunzi Salum Mnagwe.


JUMUIYA ya chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirkiana na Benk ya CRDB imemzawadia mwanfunzi mwenye ulemavu wa miguu Salum Mnagwe pikipiki ya tairi tatu(bajaji) yenye thamani ya shilingi mil.6.1 kutokana na mwafunzi huyo kuonyesha jitihada mbalimbali alipokuwa chuoni hapo.

Akimkabidhi pikipiki hiyo jana ,Makamu Mkuu wa chuo cha Mzumbe Prof.Joseph Kuzilwa alisema kuwa mwanafunzi huyo alionyesha jitahada nyingi sanaalipokuwa chuoni hapo has kuonyesha kwa jamii jinsi gani ya kuwajali watu wenye ulemavu

Prof.Kuzilwa alisema kuwa kijana salumu muda wote wa miaka mine alipokuwa chuoni hapo alishirikia katika shughuli mbalilmbali walizokuwa wanafanya wanfunzi wenzake bila kujali ulemavu wake na kuwa kama mfano kwa walemavu wenigine na jamii inayomzunguka

Alisema kuwa jumiya ya mzumbe kwa kushirikiana kwa pamoja wafanykazi na baadhi ya wanafunzi na benki ya CRDB waliona ni jambo la busara kumtafutia mwanfunzi huyo aliyehitimu masomo yake pikipiki ambayo itamsaidia katika kutoka sehemu moja kufanya kazi zake

Kwa upande wake Mwakilishi wa benki ya CRDB,Issa Singano alisema kuwa wao walipopata taarifa za kijana salumu walichukua suala hilo na kulifanyia kazi mapema kutokana na mtindo wa benki hiyo ya kujali sana maslahi ya jamii na wateja wake kwa jumla

Singano alimtaka mwanafunzi huyo mhitimu kutumia pikipiki salhiyo katika matumizi mazuri na kukitunza ili kuweza kudumu na kumsadia kwa kipindi cha muda mrefu anapokuwa katika shughuli zake za utafutaji wa maisha.

Mwanafunzi Salum Mnangwe ni mlemvua wa miguu ,amehitimu mafunzo ya taeknolojia ya habari  kwa miaka minne katika chuo kikuu mzimbe morogoro.

Mwisho

No comments:

Post a Comment