Tuesday, August 25, 2015

WAFANYABIASHARA WADOGO MOROGORO WAPEWA SOMO

Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Morogoro akiongea na wafanyabiahara wadogo,hawaonekani pichani.

SERIKALI imewataka wafanyabiashara wadogo kuacha kufanya biashara kwa mazoea bila kuwa na mawazo ya maendeleo ya baadae wakati serikali ikijipanga kuhakikisha inawalinda na kuwapatia maeneo muhimu ya kufanya biashara zao

Kauli hiyo imetolewana Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro,Noel Kazimoto wakati akifungua semina ya Kuwajengea uwezo na kuwarasimisha wafanyabiashara wadogo wadogo iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti ya Vyuo Vikuu vya Africa Mashariki na kusini (ESAURP)
Kazimoto alisema mkoa wa morogoro una wimbi kubwa la vijana ambao hawana ajira rasmi,na kujihusishana vitendo viovu,kukaa vijiweni na kufanyabiashara haramu kutokana na kukosa elimu ya ujasiriamali na wengine kukosa mitaji
Aliwataka washiriki wa semina hiyo kuwa mabalozi katika maeneo wanayotoka ili kuweza kuwabadilisha wafanya biashara wenzao kuacha kufanya biashara bila kufuata taratibu na pia kufanya biashara katika maeneo yaliyotengwa na serikali
Kwa upande wake,Mkurugenzi wa ESAURP,Prof.Ted Maliyamkono ili wafanyabiashara kusonga mbele lazima watambulike na serikali kwa kusajiliwa,kulipa kodi na kuweza kuwa na cheti cha kinatambulika na kuweza kupata mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha ama mifuko ya jamii

Pro.Maliyamkono alisema wafanyabiashara wadogo Tanzania wako zaidi ya bilioni 4,na katika utafiti wao waligundua wanakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo kutotambuliwa na serikali,kufanya biashara bila kuwa na leseni,huku biashara hizo zikifanyika katika maeneo sio rasmi.

Nae Meneja wa Mradi,ESAURP,Florentina Sallah alisema mradi huo unatekelezwa katika mikoa kumi,na lengo nikufikia watu 1500 na kila mkoa wafanyabishara 150 wanapatiwa elimu ya kutunza kumbukumbu ya biashara,mipango mikakati ya biashara,na jinsi ya kupata huduma katika taasisi za fedha na mifuko ya kijamii.

Mfanyabiashara Joyce Mhamaka alisema kuwa wajasiriamali wengi wanakabiliwa na changamoto ya mitaji,kutokuwa na elimu endelevu ya biashara,kutokuwa na leseni na sehemu rasmi ya kufanya biashara na kujikuta mara nyingi wanakimbizana na mgambo wa mji.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment