Monday, October 15, 2012

MFUKO WA BIMA YA AFYA WA TAIFA (NHIF) WAZURU ZAHATI YA CHUO KIKUU CHA KILIMO SUA



Baadhi ya Wafanyakazi wa Bima ya afya wakimsikiliza Mkurugenzi wa Afya wa SUA kabla ya kukabidhi vifaa walivyotoa katika zahanati ya Mazimbu.

 Wafanyakazi wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) wakiwa katika picha ya pamoja na wauguzi wa  zahanati ya Mazimbu-Morogoro
                                                   Mkurugenzi wa Utumishi na utawala wa mfuko wa Bima ya Afya,
                                                   Beatus Chijumba akionyesha shuka walizotoa katika zahanati ya
                                                    Mazimbu
Mkurugenzi wa Mfuko wa bima ya Afya ya Taifa (NHIF) akimkabidhi Mkurugenzi wa Afya wa Chuo Kiku cha Kilimo (SUA)  mashuka na baadhi ya vifaa vya kutoa huduma ya afya


JAMII imetakiwa kutumia rasilimali zinazowazunguka kujiunga na mifuko ya bima ya afya badala ya kuondokana na dhana ya kujiona kwamba ni maskini hivyo hawawezi kujiunga na mifuko hiyo jambo ambalo linawasababisha kushindwa kupata huduma nzuri katika vituo vya afya na zahanati pindi wanapopata matatizo.

Afisa habari mwandamizi wa mfuko wa bima ya afya(NHIF) Luhende Singu alisema hayo wakati wakikabidhi misaada kwa hospitali ya Mazimbu inayomilikiwa na chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine(SUA) ambapo wakikabidhi ,shuka 40zenye thamani ya shilingi 280,000 pamoja na miswaki,sabuni,dawa za mswaki,mataulo madogo,juisi vyote vikiwa na thamani ya shilingi 500,000.

Singu alisema kuwa jamii nyingi za kitanzania  wamekuwa wakishindwa kujiunga na mifuko ya bima ya afya ikiwemo mfuko wa afya ya Jamii (CHF) na mfuko wa bima ya afya NHIF kwa kisingizio cha kujiona kwamba maskini wakati wangeweza kutumia rasilimali walizonazo kupenda kuzitumia kikamilifu.

“jamii ni vyema ikatambua kuwa suala la afya ni muhimu kujiwekea akiba kwani mtu anaweza kuumwa na kipindi  hicho akawa hana fedha kabisa za kuweza kujitibia au kutibia familia  lakini akiwa mwanachama wa CHF na familia  au mwanachama wa  NHIF anatibiwa kulingana na uwanachama wake hata kama huna fedha”aliongeza kusema

Kwa upande wake Mkurugenzi wa utumishi na utawala wa  NHIF,Beatus Chijumba alisema kuwa NHIF licha ya wanachama wake kuchangia huduma  lakini wamekuwa wakitoa huduma hizo bure kwa makundi maalum wakiwemo wazee,watoto yatima wajawazito wanaotoka katika familia maskini pamoja na familia zao .

Chijumba alisema mpango huo umeanza tangu mwaka jana na kwamba wananchi katika mikoa ya Lindi naTanga ambako wameanza nako wamefaidika na huduma hiyo kwa lengo la kusaidia jamii katika suala zima la huduma ya afya na jamii ya watanzania ituunge mkono katika zoezi hili kwani lengo ni kuhakikisha huduma nzuri inapatikana kwa wakati muafaka

Alisema wameamua kutoa msaada kwa hospitali ya Mazimbu kwa kuwa pamoja na kutoa huduma kwa jamii lakini wamebaini huduma za afya zimekuwa zikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo vifaa vya  tiba,madawa  na mengine hiyo msaada huo utasaidia katika kuhudumia wagonjwa pindi wanapofika kupata huduma katika zahati hiyo

Mkurugenzi wa huduma za afya katika chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA),dk Omari Kasuwi mara baada ya kupokea vifaa hivyo alisema kuwa hospitali hiyo ina dawa za kutosha za kuhudumia wagonjwa lakini wanakabiliwa na changamoto za kutokuwa na baadhi ya vipimo hivyo kulazimika kuwapeleka katika hospitali za rufaa kama Muhimbili na kwingineko kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Dk Kasuwi alisema hospitali hiyo inapokea wagonjwa kati ya 150 hadi 200 kwa siku wenye matatizo mbalimbali yakiwemo ya ugonjwa moyo,malaria,kansa na kwamba wanalaza wagonjwa lakini wamekuwa wakiombwa na jamii kutoa huduma ya chakula hospitalini hapo ambapo kwa hilo chuo kinajipanga kulifanyia kazi.

No comments:

Post a Comment