SHIRIKA lisilo la kiseriklia la tanZED la nchini Ireland limetoa msaada wa kompyuta 25 katika shule ya sekondari ya Mbuyuni iliyopo manispaa ya Morogoro kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kufahamu matumizi kompyuta tangu wakiwa sekondari ili kupambana na changamoto zinazowakabili
Makamu
mkuu wa shule hiyo ya sekondari Mbuyuni Festo Kayombo alisema kuwa shirika hilo
limetoa msaada huo baada ya kuridhishwa na utawala wa shule hiyo na hivyo
kuamua kutoa kompyuta hizo ikiwa ni programu ya shirika hilo kusambaza
kompyuta kwa shule za sekondari nchikwa lengo la kuendeleza sekta ya elimu
Kayombo Alisema
kuwa shule hiyo baada ya kutapa msaada huo imeanza utaratibu wa kutoa mafunzo
ya Kompyuta kwa awamu kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambao wanatarajiwa
kumaliza ili wamalizapo wawe na uelewa watakapo endelea na msomo ya juu.
Kayombo alisema
pamoja na kupata msaada huo uongozi wa shule utashirikiana na uongozi wa kata
ya Mbuyuni kuhakikisha jamii inayozunguka shule hiyo kujifunza kwa utaratibu
utakaopangwa ili na jamii hiyo iweze kunufaika na mradi huo.
Kwa upande
wake diwani wa kata ya mbuyuni Samueli Msuya akikabidhi msaada huo
aliwataka wanafunzi wa shule hiyo kutumia kompyuta hizo kwa matumizi
yaliyokusudiwa na si vinginevyo kulingana na walimu wao wanavyowaelekeza
Aliwataka
walimu na uongozi wa shule kusimamia kikamilifu na kuvitunza vifaa hivyo ili
kuweza kukaa kwa muda mrefu na kuweza kuwasaidia wanafunzi wanaoingia shuleni
hapo kila mwaka kuweza kufaidika pia.
Msuya
alisema lengo ni kuhakikisha kila mwanafunzi anaemaliza anafahamu kutumia kompyuta
kwa lengo la kuendana na utandawazi na
kuweza kufanya vizuri watakapoendelea na elimu ya juu kutokana na vyuo
vingi wanasoma kwa njia ya tovuti
No comments:
Post a Comment