Saturday, October 20, 2012

CHUO KIKUU HURIA CHATOA MSAADA WA MASHUKA HOSPITALI YA OCEAN ROAD


Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania-OUT- imetoa msaada wa mashuka kwa wagonjwa wa hospitari ya wa saratani  ya Ocean road jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya  maadhimisho ya miaka 20 ya chuo kikuu hicho nchini tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992

. Akikabidhi msaada huo Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania OUTSO ndugu JOHN MLAGULA amesema msaada huo ni kutambua mchango na huduma inayotolewa na hospitali ya ocean road katika utoaji huduma za kiafya kwa wagonjwa wa saratani nchini.

Amesema katika maadhimisho hayo open university students organisation outso imekabidhi mashuka 110 kwa oungozi wa hospitali ya ocean road ili kuboresha huduma kwa wagonjwa wanao hudumiwa.

Hatahivyo rais huyo wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu huria ameahidi kuchanga michango kila mwaka kutenga siku maalumu kwa ajili ya kupeleka msaada wa hali na mali katika hosopitali hiyo

.Naye muuguzi mkuu wa hospitali ya ocean road ndugu MARY HAULE ameshukuru kwa msaada huo na kuhimiza watanzania wengi kuchangia kwa kutafutia ufumbuzi wa mahitaji mbalimbali ya hospitali hiyo inayohudumia watanzania wengi.

No comments:

Post a Comment